Quantcast
Channel: TZhiphop » Artist of The Week
Viewing all articles
Browse latest Browse all 10

Kalapina ndani ya FidStyle Friday

$
0
0

Kikosi cha Mizinga ni mojawapo ya makundi muhimu mno ambayo yamekuwa yakiendelea kuwa na sauti muhimu kwenye medani ya Hip Hop Tanzania, huku wakiwa wameegemea zaidi kwenye kuwasilisha vilio vya watu wa tabaka la chini dhidi ya “wanyonyaji”.  Kikiongozwa na Kalapina, Kikosi  kimeendelea kujikusanyia wafuasi — tofauti na mashabiki — nchini na nchi za jirani, wakirusha mawimbi kutoka Block 41, Kinondoni, Dar es Salaam.

Katika kipindi cha FidStyle Friday cha wiki hii, tunapata fursa ya kusikia kutoka kwa Kalapina tena, akirusha mabomu kuelekea kwenye mifumo ya siasa. Pia, wasanii kama Zimwi, Aboo Gaidi na Onya Man, kutoka Kikosi Records, wanahakikisha ile sauti na nguvu inayohusishwa na Kikosi inasikika na kuonekana.  Fid Q na Kalapina wanajadili mambo kadhaa nyeti, kuanzia matatizo ya hati miliki hadi sanaa ya uandishi au ushairi — kuandika ambacho unahisi au kuandika unachofikiri?

Makala na kurasa zaidi kuhusu Kikosi:


Viewing all articles
Browse latest Browse all 10

Trending Articles