Baada ya Cliff Mitindo kuwakilisha Migo Migo, wiki iliyofuata ilikuwa ni ya mkongwe JCB. Wanaomfahamu vizuri JCB nadhani watashauri ujiandae kupokea hadithi za kitaa kama zilivyo. Kama Mejah wa Wachata Crew anavyosema, JCB amekuwa akilinda ngome ya Kijenge Juu toka mwaka 1996, akihakikisha familia ya Watengwa inaendelea kufanya kile kinachotakikana — kuwakilisha mitaa, hasa Kijenge Juu.
Akionesha uzoefu wa hali ya juu mbele ya kipaza, anahakikisha kila mtu anajua kuwa yeye ndio yupo ndani ya nyumba! Lakini wakati huo huo anaambatana na taswira za kitaa, maneno yake yakiwa lenzi inayokuonesha kila kitu kinachoendelea Kijenge Juu (Donnie, familia ya Watengwa na Hip Hop Tanzania wanakusubiri).
Pia, JCB anatumia fursa hii kujadili mikakati yake na mipango ya Watengwa — “Ni Full Ile Laana Vol 2″ inakaribia kuingia kitaani — bila kusahau S.U.A. Kikosi cha CheusiDawaTV kitawatembelea Watengwa na kumhoji Daz Naledge ili kutupa undani na maendeleo ya mradi mzima.
Hadithi za kitaa…
Makala nyingine kuhusu JCB na Watengwa: