Quantcast
Channel: TZhiphop » Artist of The Week
Viewing all articles
Browse latest Browse all 10

Nikki Mbishi ndani ya FidStyle Friday

$
0
0

Hiki ni kipindi cha 30 tangu maneno “FidStyle Friday” yalipoanza kusambaa kwenye mtandao. Katika kusheherekea hatua hii muhimu, ni vyema kuangalia kilichokuwa kinajiri awali.

Nikki Mbishi alikuwa ni msanii wa kwanza kualikwa, na anaalikwa tena ili kutumia darubini yake kuangalia safari ilipoanzia. Kama kawaida, Nikki hajaharibu; anafungua kwa Sauti ya Jogoo kuamsha jamii nzima ya Tanzania, kuanzia tabaka la juu mpaka la chini kabisa na kukumbusha watu majukumu yao. Mfalme wa “underground mainstream” pia anaongelea jinsi uhalisia, na wasanii wanaoakisi uhalisia, unavyowapa taswira bora mbele ya hadhira na jamii kwa ujumla.

Ukiacha mjadala na Fid Q kuhusu Hip Hop na sanaa Tanzania, Nikki anaonesha kipaji alichonacho cha kutunga na kuwasilisha ushairi. Ingawa kuna wakati anaongelea mambo ambayo labda hayajadiliwi au hayaongelewi kwa “uwazi”, ni wazi kuwa Nikki anajua anachofanya. Msikilize kwa makini jinsi anavyocheza na maneno. Mfano mzuri ni mstari huu kutoka kwenye wimbo Kilinge: “Hata ukiwa na mvi Shirazi unahitaji Afro.” Au: “Nageuka Oliver, Mtukudzi namwimbia Tobi na Neria.” Unaweza ukadhani anasema, “Nageuka Oliver, mdokozi namwibia Tobi na Neria!”

Mistari kama hiyo ya kutega akili ipo mingi tu, kwa hiyo mtegeee sikio huyu Drosophila melanogaster kwa makini. Mtiririko wa maneno yafuatayo kwenye mojawapo ya beti anazowasilisha utakuacha unatingisha kichwa: “Nini Chanzo… Hili Game… Juma Nature.”

Taarifa na makala zaidi kuhusu Nikki Mbishi:


Viewing all articles
Browse latest Browse all 10

Trending Articles